Karibu kila mtu katika nyakati fulani hufikiria biashara za kufanya au njia za kutengeza pesa ambazo zitamletea pesa hata wakati wa usiku akiwa amelala. Hii maana yake ni kwamba biashara huingiza pesa hata kama mmiliki wa hiyo biashara hatakuwepo pale. Biashara nyingi humlipa yule mwenye biashara kulinganna na masaa anayotumia kuitumikia biashara husika. Unaweza kuona sasa kwamba biashara ya namna hiyo haina tofauti kubwa na ajira ya kawaida. Kuna dhana iliyojengeka kwamba njia kubwa ya kuingiza pesa hata ukiwa umelala usiku wa manane ni kwa kupitia mtandao wa intaneti tu peke yake/biashara za mtandaoni au wengine mara nyingi huiita, njia ya kutengeneza pesa kupitia blogu . Lakini kiuhalisia mtu unaweza ukatengeneza pesa hata ukiwa umelala kwa kupitia biashara yeyote ile ilimradi tu umetengeneza mfumo(system) imara utakaowezesha shughuli kufanyika hata kama haupo pale. Hebu fikiria mmiliki wa mgahawa mkubwa wenye wafanyakazi kila idara kuanzia meneja mpaka mfagiaji, ana haja ya ku...
Comments
Post a Comment